SERGIO RAMOS AJIUNGA RASMI PSG


Sergio Ramos (35) amesaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya PSG ya Paris akitokea Real Madrid ya Uhispania ambako amekaa kwa miaka 16.

Paris St-Germain imemsajili Sergio Ramos kwa kandarasi ya miaka miwili baada ya mchezaji huyo kuondoka katika klabu yake ya miaka mingi Real Madrid.

Ramos , 35 aliondoka Madrid baada ya miaka 16 wakati kandarasi yake ilipokamilika mwisho wa mwezi Juni.

Akiwa klabuni hapo ameshinda mataji ya Klabu Bingwa (4), La Liga (5) na Klabu Bingwa ya Dunia (4)

Mchezaji huyo ambaye ameichezea mara nyingi zaidi timu yake ya taifa kushinda mchezaji yeyote yule ,ameshinda mataji matano ya La liga na mataji manne ya kombe la klabu bingwa akiichezea Real Madrid.


Ruka Twitter ujumbe, 1

Mwisho wa Twitter ujumbe, 1


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments