NAIBU WAZIRI MARY MASANJAAFANYA ZIARA KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII WILAYANI SONGEA


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimsikiliza Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji na ya Kumbukumbu ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa, Balthazar Nyamusya (kushoto) akitoa maelezo kuhusu zana za mishale zilizotumika kipindi cha vita ya Majimaji, alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua eneo la Makumbusho ya Majimaji lililopo Bombambili Wilaya ya Songea.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimsikiliza Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji na ya Kumbukumbu ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa, Balthazar Nyamusya (kushoto) akitoa maelezo kuhusu handaki lililopo kwenye Makumbusho ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua eneo hilo lililopo Bombambili Wilaya ya Songea .
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akimsikiliza Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji na ya Kumbukumbu ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa, Balthazar Nyamusya (kulia) akitoa maelezo kuhusu mavazi yaliyopo kwenye Makumbusho ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa, wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua Makumbusho hiyo iliyopo eneo la Bombambili Wilaya ya Songea.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akiangalia mnara wa kumbukumbu waliponyongwa mashujaa wa Vita vya Majimaji alipofanya ziara ya kikazi ya kukagua eneo hilo lililopo Wilaya ya Songea. Kulia ni Mhifadhi wa Makumbusho ya Majimaji na Makumbusho ya Kumbukumbu ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa, Balthazar Nyamusya.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akiongoza msafara kupanda Mlima Matogoro katika Hifadhi ya Misitu ya Milima ya Matogoro iliyopo kwenye Manispaa ya Songea. Nyuma yake ni Kamishna Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof. Dos Santos Silayo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments