MUFTI WA TANZANIA ASEMA SIKUKUU YA EID EL-ADH’HAA ITAKUWA 21 JULAI 2021

Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir ametangaza kuwa Sikukuu ya Eid El-Adh’haa itakuwa Julai 21, 2021, ambapo itakuwa siku ya mapumziko kitaifa.

Taarifa ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) imeeleza kuwa maadhimisho ya sikukuu hiyo kitaifa yatafanyika mkoa wa Dar es Salaam ambapo swala itafanyika katika Msikiti wa Mtoro na Baraza la Eid litafanyika hapo hapo.

Mufti ametumia nafasi hiyo kuwatakia Waislam na Watanzania wote sikukuu njema na amewaomba kusherehekea kwa usalama na amani huku wakiendelea kuchukua tahadhari dhidi ya UVIKO-19.


 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments