MREMBO AMUUA MPENZI WAKE KWA KUMFUNGIA NDANI KISHA KUCHOMA MOTO NYUMBA DAR


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Muliro Jumanne,

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, linamshikilia Grace Mushi (25) kwa tuhuma za kumuua aliyekuwa mpenzi wake Khamis Abdallah (25), mkazi wa Mbezi Makabe baada ya kumfungia ndani ya nyumba na kuimwagia mafuta ya petroli na kisha kuichoma moto nyumba hiyo.

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo Muliro Jumanne, na kusema kuwa tukio hilo limetokea Julai 16, 2021, majira ya saa 8:30 usiku na uchunguzi umebaini kwamba wapenzi hao walikuwa na mgogoro mkubwa wa mapenzi.

"Baada ya tukio hilo mtuhumiwa alijaribu kutoroka lakini kwa kushirikiana na wananchi alikamatwa na uchunguzi wa awali umeonesha kwamba ulikuwepo mgogoro mkubwa wa kimpenzi kabla ya kufanyika kwa tukio hili la mauaji ya kikatili," ameeleza Kamanda Muliro.

CHANZO - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments