SERIKALI YASEMA IPO TAYARI KUKUTANA NA MANABII WANAODAI KUFUFUA WAFU



Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi imesema kuwa ipo tayari kukutana na manabii wanaodai kuweza kufufua wafu ili iweze kuwaelimisha na kuwaelekeza kuwa mwenye uwezo wa kuchukua na kurejesha ni Mungu pekee.

Kauli hiyo imetolewa hii leo Mei 17, 2021, Bungeni Dodoma, na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Hamza Chilo, wakati akijibu swali la Mbunge wa Mtambwe kupitia Chama cha ACT-Wazalendo Khalifa Mohamed Issa, aliyehoji umuhimu wa serikali kukutana na wale manabii wanaodai kuweza kufufua wafu ili waweze kuwafufua wapendwa wao.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post