RAIS SAMIA APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI 5 WALIOTEULIWA KUZIWAKILISHA NCHI ZAO HAPA NCHINI

 

Rais Samia Suluhu Hassan leo amepokea hati za utambulisho za Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.

Mabalozi waliowasilisha kwa nyakati tofauti hati zao za utambulisho kwa Rais Samia Suluhu Hassan wanatoka katika nchi za Namibia, Msumbiji, Uturuki, Italia na Ireland.

Tukio la Rais Samia Suluhu Hassan kupokea hati hizo za utambulisho kutoka kwa Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini limefanyika Ikulu jijini Dar es salaam, na kushuhudiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula.

Baada ya kupokea hati hizo za utambulisho, Rais Samia Suluhu Hassan kwa nyakati tofauti amefanya mazungumzo na Mabalozi hao.


 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments