WAZIRI AWESO AWASHA MOTO MOROGORO AMTUMBUA KIGOGO WA MORUWASA

 


 

Na Mwandishi,Morogoro

  

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso amewasimamisha kazi vigogo wa Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Morogoro (Morowasa) ili kupisha uchunguzi wa wa tuhuma ambazo zinawakabili huku akiagiza watumishi wengine kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

 

Vigogo waliosimamishwa kazi kupisha uchunguzi ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA) Mhandisi Tamimu Katakweba,Afisa Maji wa Bonde la Wami Ruvu Bwana Simon Ngonyani huku akiagiza watumishi wengine waliokuwa vinara wa kueneza chuki na kuleta taharuki badala ya kufanya kazi nao wachukuliwe hatua za kinidhamu.

 

Waziri Aweso aliyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara yake ya kikazi mkoani Morogoro ambapo alisema kuwa Mkurugenzi wa Moruwasa pamoja na tuhuma nyingine za kiutumishi lakini alisaini mkataba wa fedha nyingi na wakandarasi bila kushirikisha Wizara na hata bila uwepo wa Katibu Mkuu kinyume na taratibu.

 

Huku Afisa  wa Bonde akisimamishwa kupisha uchunguzi wa tuhuma za ukiukwaji wa maadili ya utumishi.

 

Mwisho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments