RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA MKUU WA ITIFAKI NA MKURUGENZI MKUU WA eGA


 Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Yusuf Mndolwa kuwa Balozi.

Pamoja na uteuzi huo, Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Mteule Mndolwa kuwa Mkuu wa Itifaki (Chief of Protocol) katika wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Mteule Mndolwa anachukua nafasi iliyoachwa na Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Balozi Mteule Mndolwa ataapishwa Jumatatu aprili 19, Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.

Wakati huo huo Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Benedict Ndomba kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA).

Kabla ya uteuzi huo Ndomba alikuwa Mkurugenzi wa Miundombinu na Operesheni wa eGA na anachukua nafasi ya Dkt. Jabir Kuwe ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Uteuzi wa viongozi hao umeanza Aprili 17, 2021.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments