MWADUI FC YATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA TFF BAADA YA KUICHARAZA COASTAL UNION 2-0


TIMU ya Mwadui FC imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Coastal Union ya Tanga jioni ya leo Uwanja wa Mwadui Complex, Kishapu mkoani Shinyanga.

Mabao ya Mwadui FC yamefungwa na Roshwa Rashid dakika ya 14 na Wallace Kiango dakika ya 24.
Mwadui FC inakamilisha orodha ya timu tatu tupu za mikoa inayopakana kufuzu Robo Fainali hadi sasa, nyingine ni Biashara United ya Mara na Rhino Rangers ya Tabora.

Mchezo kati ta wenyeji, Tanzania Prisons na Yanga SC unafuatia hivi sasa Uwanja wa Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.
 Via Binzubeiry

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments