KAMATI YA BUNGE YASHAURI ASKARI WAHAMISHWE URAIANI


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje Ulinzi na Usalama imeishauri  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na Jeshi la Polisi nchini  kutumia Mfumo wa Fedha za Tuzo na Tozo katika kuendesha miradi mbalimbali ya jeshi hilo ambayo uzoefu unaonyesha miradi  mingi iliyotumia fedha hiyo kukamilka huku kamati hiyo ikisisitiza ujenzi wa nyumba za askari ili kuwaondoa askari polisi uraiani.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo,ambaye pia ni Mbunge wa Ilala,Mussa Azan Zungu baada ya ukaguzi wa miradi miwili ya Jeshi la Polisi ikiwemo Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida na Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Kikosi cha FFU Pamoja na ghala la silaha.

“Mtumie Mfuko wa Tuzo na Tozo kujenga nyumba za maafisa na askari,mpunguze maaskari kukaa uraiani,wakikaa uraiani kuna matatizo makubwa wanazoeana sana na wananchi na askari eneo lake ni kambini sio kukaa nje ya kambi” alisema Zungu

Mbunge Zungu pia alitumia fursa hiyo kumpongeza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene na Inspekta Jenerali wa Polisi,Simon Sirro kwa kusimamia Pamoja na kukamilisha miradi mbalimbali ndani ya jeshi hilo.

Akizungumza katika ziara hiyo,Mshauri wa Ujenzi wa Jeshi la Polisi nchini,Naibu Kamishna Richard Malika alitaja gharama ya Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Kamanda ambapo mpaka mradi kukamilika utagharimu Shilingi Bilioni 1.2 huku akiweka wazi gharama hizo kutoka katika mfuko wa tuzo na tozo uliopo chini ya Inspekta Jenerali wa Polisi,Simon Sirro.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments