NAIBU SPIKA DKT TULIA AZINDUA KAMPENI YA KUCHANGIA UJENZI WA HOSTELI ZA WANAFUNZI WA KIKE CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA (CBE) KAMPASI YA MBEYA


Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson (katikati), Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe (kushoto) pamoja na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Profesa Emmanuel Mjema (kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kuzindua Kampeni ya harambee ya kuchangia ujenzi wa hosteli za Wanafunzi wa Kike Chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya uliofanyika Serena hotel mkoani Dar es Salaam.Mradi huo ambao utagharibu zaidi ya bilioni moja kampeni yake itaendelea kufanyika ndani ya siku 90 kwa lengo la kuhakikisha fedha hizo zinapatikana.
Mgeni rasmi Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson (katikati), Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe (kushoto) pamoja na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Profesa Emmanuel Mjema (kulia) wakizindua Kampeni ya harambee ya kuchangia ujenzi wa hosteli za Wanafunzi wa Kike Chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya uliofanyika Serena hotel mkoani Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson akizungumza na wadau wa Elimu, Wanafunzi waliosoma chuo cha CBE (Alumni) pamoja na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu namna ujenzi wa hosteli hizo zitakavyoweza kuwasaidia na kuwapunguzia adha Wanafunzi wa Kike wawapo masomoni katika kampasi ya CBE Mbeya.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe akizungumza kuhusu namna Serikali ilivyojipanga kuhakkisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo hasa kwenye sekta ya Elimu ya Biashara wakati wa uzinduzi Kampeni ya harambee ya kuchangia ujenzi wa hosteli za Wanafunzi wa Kike Chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya uliofanyika Serena hotel mkoani Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Profesa Emmanuel Mjema akizungumza kuhusu namna CBE walivyojipanga kusimamia mradi wa ujenzi wa hosteli za Wanafunzi wa Kike katika chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya utakaogharimu takribani bilioni moja. Uzinduzi wa kampeni hiyo utaendelea kufanyika ndani ya siku 90 kwa lengo la kuchangisha fedha hizo kwa ajili ya kujenga mabweni hayo.

Baadhi ya wadau wa Elimu pamoja na wanafunzi waliosoma chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi wakati wa uzinduzi waKampeni ya harambee ya kuchangia ujenzi wa hosteli za Wanafunzi wa Kike Chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya uliofanyika Serena hotel mkoani Dar es Salaam.
Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson , Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe pamoja na Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara(CBE) Profesa Emmanuel Mjema wakipita meza moja baada ya nyingine kwa ajili ya kufanya harambee mara baada ya uzinduzi wa kampeni ya siku 90 yenye lengo la kuchangisha takribani bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa hostel za Wanafunzi wa kike katika chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya.

Naibu Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Emmanuel Munishi akizungumza wakati akiwakaribisha wageni waalikwa mbalimbali akiwemo Mgeni rasmi waliofika kwenye hafla hiyo adhimu ya uzinduzi wa kampeni ya siku 90 yenye lengo la kuchangisha takribani bilioni moja kwa ajili ya ujenzi wa hostel za Wanafunzi wa Kike kike katika chuo cha Elimu ya Bishara (CBE) kampasi ya Mbeya.
Muendesha shughuli wa hafla nzima alikuwa ni mmoja wa Ma-MC maarufu mkoani Dar Es Salaam Athony Luvanda.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments