BLOGGER SHAMIMU MWACHA NA MMEWE WATUPWA JELA MAISHA


Mahakama Kuu kitengo cha Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, maarufu kama Mahakama ya Mafisadi, imemhukumu blogger Shamimu Mwasha (41), na mume wake Abdul Nsembo, maarufu kama Abdulkandida (45) kutumikia kifungo cha maisha gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na dawa za kulevya aina ya Heroine.

Hukumu hiyo imetolewa leo Machi 31, 2021 na Jaji Elieza Luvanda baada yaa kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo na mashahidi sita wa upande wa mashtaka.

Shamimu anayemiliki Blog ya 8020 na mumewe Nsembo, walikuwa wanakabiliwa na
mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroini gramu 439.70, kosa wanalodaiwa kulitenda Mei mosi 2019 huko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam.

CHANZO- MICHUZI BLOG

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments