RAIS MWINYI ATEUA WANACHAMA WA ACT WAZALENDO KUWA MAWAZIRI


Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Mwinyi, amewateua wanachama wawili wa Chama cha ACT-Wazalendo, Omar Said Shaaban na Nassor Ahmed Mazrui kuwa mawaziri.

Kushoto ni Omar Said Shaaban, aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda na kulia ni Nassor Mazrui, aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Afya.

Uteuzi huo umeanza hii leo Machi 3, 2021, ambapo Omar Shaaban, ameteuliwa kuwa Waziri wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda huku Nassor Mazrui, ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto.

Mwingine aliyeteuliwa leo ni Dkt. Saada Mkuya Salum, kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na wote kwa pamoja wataapishwa kesho Machi 4.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments