ASKOFU MAKALA AONGOZA MAOMBI YA SIKU TATU YA KUTUBU NA KUIOMBEA NCHI NA WATANZANIA KWA MUNGU AEPUSHE UGONJWA WA CORONA

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Dkt. Emmanuel Makala 

***

Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria Dkt. Emmanuel Makala amewaongoza waumini wa kanisa hilo Usharika wa Ebenezer mjini Shinyanga katika uzinduzi wa siku tatu mfululizo za kufunga na kuomba zinazoenda sambamba na siku 40 za mfungo wa Kwaresma kwa lengo la kuitikia wito wa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwataka Watanzania kufanya maombi ya kuliombea taifa kwa mwenyezi Mungu awaepushie Watanzania ugonjwa wa Corona.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maombi hayo Askofu Dkt. Emmanuel Makala amesema kiongozi wa nchi anapoagiza kitu au anapotoa rai wa wananchi asiyepokea na kutii atakuwa anapingana na ofisi na siyo mtu kwa hiyo yeye ameitikia wito wa kiongozi wa nchi na kuwataka waumini wa dini ya kikristo pamoja na dini zingine kuungana na Watanzania wengine kuomba na kuliombea taifa kwa mwenyezi Mungu kuiepusha nchi na ugonjwa huu wa Corona.

Aidha Chaplain wa Kanisa Kuu la Ebenezer na Mchungaji Kiongozi Mch. Odolous Gyunda amesema lengo la maombi ya siku tatu mfululizo ni kutubu na kuabudu kwa ajili ya nchi ya Tanzania na kumuunga mkono kiongozi wa nchi na maombi hayo yanayoambatana na nyimbo za kusifu na kuabudu yataendelea kwa muda wa siku 40 za Kwaresma.

Baadhi ya waumini walioshiriki katika ibada hiyo ya maombi wamesema wanamuona Mheshimiwa Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kama mfalme wa Ninawi enzi zile alipopiga mbiu kumlilia Mungu na kuomba toba kwa hiyo sauti aliyoutoa Rais ni sauti ya Mungu kwa ajili ya kuliokoa taifa la Tanzania.

Naye Katibu wa Dayosisi Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria bi. Happyness Gefi kama kungelikuwa na namna rahisi ya kuponyesha ugonjwa wa Corona basi mataifa makubwa yenye nguvu na uwezo yangekuwa yameshatokomeza ugonjwa huo kwa uwezo wa kiuchumi walio nao lakini lakini kwa kuwa ugonjwa huo haubagui tajiri wala masikini ni jambo la kumshukuru mungu sana kwa maono aliyo nayo lakini pia shukrani kwa Askofu Emmanuel Makala kwa kuona umuhimu wa kupokea wito wa mkuu wa nchi na kushusha chini kwa waumini kutekeleza kwa vitendo kwa nia moja na kwa dhati ya mioyo yao.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments