AMUUA DADA YAKE KWA PANGA UGOMVI WA HELA YA NYANYA


Picha ya nyanya
**
Na Mwandishi wa Malunde 1 blog
Mkazi wa kijiji cha Urauri ,kata ya Reha wilayani Rombo mkoa wa Kilimanjaro Magreth Mushi ameuawa kwa kukatwa Panga 'kitu chenye ncha kali' kichwani na kaka yake aitwaye Neoni Lazaro kwa madai ya kugombania fedha alizouza nyanya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Ronald Makona amesema tukio hilo limetokea Februari 9, 2021 saa tatu usiku katika kijiji cha Urauri kata ya Reha wilayani Rombo.

Amesema Magreth alifariki dunia usiku huo wa kuamkia Februari 10 alipopelekwa katika Hospitali ya Huruma kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments