Tanzia : ALIYEKUWA GAVANA WA BENKI KUU YA TANZANIA PROF. BENNO NDULLU AFARIKI DUNIA


Profesa Benno Ndullu enzi za uhai wake
***
Aliyewahi kuwa Gavana Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu (71) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Februari 22,2021 katika hospitali ya Hubert Kairuki Memorial University alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.

Katibu muhtasi wake, Msafiri Nampesya ameithibitisha kuhusu kifo hicho.

Profesa Ndullu alikuwa Gavana wa Benki kuu ya Tanzania, kuanzia 2008 hadi 2018 na pia aliwahi kuwa Mhadhiri wa Uchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kwamba aliwahi kufanya kazi Benki ya Dunia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments