YANGA YAICHAPA NAMUNGO FC BAO 1-0 MICHUANO YA MAPINDUZI CUP


Baada ya kutoka sare katika mechi ya kwanza Yanga imefanikiwa kutoka na pointi tatu muhimu dhidi ya Namungo katika michuano ya Mapinduzi Cup yanayoendelea Visiwani Zanzibar baada ya kuichapa Namungo bao 1-0.

Bao la pekee la Yanga liliwekwa kimyani na Kiungo wao Zawadi Mauya mnamo dakika ya 24 ya mchezo.

Yanga ilifanya mabidiliko kadhaa ya wachezaji na kuwapumzisha wachezaji ambao walianza katika mchezo wa kwanza wa mashindano hayo.

Via Fullshangwe blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments