AKAMATWA UWANJA WA NDEGE AKISAFIRISHA VINYONGA 74



Mwanaume mwenye umri wa miaka 56 ambaye hakutambuliwa zaidi  amekamatwa na Mamlaka nchini Austria katika uwanja wa ndege wa Vienna akiwa anatorosha vinyonga 74 kutoka nchini Tanzania.

Kwa Mujibu  wa gazeti la The Telegraph la Uingereza jamaa huyo alikuwa amewaficha wanyama hao katika soksi na masanduku ya barafu alipokamatwa na maofisa forodha wa uwanja huo wa Vienna.

Naibu katibu mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii nchini Tanzania, Allan Kijazi amesema mwanaume huyo alisafiri kwenda Austria kutoka Tanzania kupitia Ethiopia na kwamba mujibu wa gazeti hilo vinyonga hao walikuwa wakipelekwa kwenye bustani ya wanyama ya Schoenbrunn na ilibainika kuwa watatu wamekufa.

Amesema wanyama wote walikuwa wanatoka katika milima ya Usambara Tanzania na walikuwa katika umri wa wiki moja hadi wakubwa ambao walitakiwa kuuzwa katika masoko ya ulanguzi.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments