MWANDISHI ALIYERIPOTI MLIPUKO WA CORONA CHINA AHUKUMIWA JELA MIAKA MINNE
Monday, December 28, 2020
Mwandishi wa habari Zhang Zhan amehukumiwa kifungo cha miaka minne kwa kuripoti mlipuko wa kwanza wa virusi vya Corona katika mji wa Wuhan. Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya Shanghai.
Mahakama ya Shanghai imechukua uamuzi kifungo cha miaka minee dhidi ya mwandishi wa habari Zhang Zhan baada ya kuangazia mlipuko wa kwanza wa virusi vya Corona, amesema mwanasheria wake.
Kwa mujibu wa mashataka yanayomkabili, alisafiri hadi Wuhan mwezi Februari kuripoti kuhusu mlipuko wa virusi bila kuzingatia kanuni zilizowekwa.
Ripoti yake aliyoweka mubashara katika mtandao wa kijamii ilivuma sana mwezi Februari, ilimweka mashakani baada ya kuvutia mamlaka za China.
Kesi yake, ambayo imefunguliwa Jumatatu hii, ilichukua saa chache kbala ya kutolewa uamuzi. Mwandishi huyo wa habari, mwenye umri wa miaka 37, alikamatwa mwezi Mei mwaka huu, akishumiwa "kuchochea vurugu" kwa kueneza "habari za uwongo".
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin