ADAIWA KUMCHINJA KAKA YAKE AKIMDAI SH LAKI 7

Picha haihusiani na habari hapa chini

Na Anthony Mayunga - Mwananchi
 Polisi wilaya ya Serengeti mkoani Mara wanamshikilia Juma Masiaga (38) mkazi wa kijiji cha Kitunguruma kwa tuhuma ya kumchinja kaka yake, Chacha (40) kwa madai ya kutomlipa Sh700,000/=.

Akizungumza na Mwananchi Digital jana Alhamisi Desemba 24, 2020 mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu amesema tukio hilo limetokea jana saa nne usiku.

"Alimvizia na kumkata shingoni na kichwani kisha akakimbia na leo amenaswa eneo la jalala kuu mjini Mugumu akijaribu kutoroka, sasa anahojiwa na polisi kwa ajili ya hatua zaidi," amesema.

Amesema taarifa zilizopo ni kuwa alikuwa akimdai kaka yake Sh700,000/= baada ya awali kulipwa Sh800,000/=.

Ofisa mtendaji wa kijiji hicho, Joseph Petro amesema hakuwahi kusikia mgogoro wowote wa ndugu hao na kwamba kama alikuwa na malalamiko angeyawasilisha sehemu husika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post