RAIS DKT. MWINYI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI MKUU WA AFYA KATIKA WIZARA YA AFYA


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Afya katika Wizara ya Afya, Dkt. Jamala Adam Taib kuanzia Novemba 18, 2020.

Aidha, Dkt. Mwinyi ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Mnazi Mmoja, Dkt. Ali Salum Ali.

Dkt. Mwinyi amefikia uamuzi huo baada ya kufanya ziara katika hospitali hiyo ili kujionea mwenyewe hali ya utoaji wa huduma na changamoto zinazoikabili hospitali hiyo.

Kufuatia utenguzi huo, Dkt. Mwinyi amesema wote ambao uteuzi hao umetenguliwa watapangiwa kazi nyingine.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments