Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewaonya baadhi ya wanasiasa nchini kuacha kuwatumia vibaya wananchi hususan vijana hasa katika kipindi hiki cha kampeni za kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 2020 na kuwaingiza kwenye vitendo vya uvunjifu wa amani.
IGP Sirro amesema hayo akiwa Musoma mkoani Mara kwenye kikao kilichowahusisha viongozi wa kisiasa wakiwemo wagombea wa nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu waliopo mkoani humo ambapo aliwataka wagombea hao kutumia majukwaa ya kampeni kuhubiri amani.
Kwa upande wake mgombea ubunge jimbo la Bunda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Ester Bulaya, amesema katika kipindi hiki cha wiki mbili kilichobaki kuelekea uchaguzi mkuu lazima vyama vishikamane na kuwa makini sambamba na kulipongeza Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin