Picha : HASHIM RUNGWE ACHUKUA FOMU NEC KUGOMBEA URAIS TANZANIA KUPITIA CHAUMA

Mwenyekiti wa Chama cha CHAUMA Hashim Rungwe, leo Agosti 10, 2020, amechukua fomu ya kuwania Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwezi Oktoba katika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), zilizopo Dodoma.

Rungwe amefika katika ofisi hizo mapema leo asubuhi akiongozana na mgombea mwenza Mohammed Masoud, na kukabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa NEC Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527