Morrison Ajiunga Na Simba Akitokea Yanga Sc

Benard Morrison kiungo mshambuliaji wa Yanga leo ametambulishwa ndani ya kikosi cha Simba.

Morrison mwenye mabao manne ndani ya Ligi Kuu Bara wakati akikipiga Yanga alikuwa kwenye mvutano mkubwa na mabosi wake kwenye suala la mkataba ambapo mchezaji alisema kuwa ana dili la miezi sita huku uongozi ukisema kuwa amesaini dili la miaka miwili.

Leo Agosti 8, Morrison amevalishwa jezi nyekundu na kuonekana akisaini dili jipya la kujiunga na Simba.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments