ZITTO KABWE NA WENZAKE 07 WARIPOTI POLISI LINDI , WATAKIWA KUREJEA TENA JULAI 20

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo , Zitto Kabwe na viongozi wengine saba wa Chama hicho wameripoti Kituo Kikuu cha Polisi Mkoani Lindi kama walivyohitajika.

Zitto pamoja na viongozi wengine akiwemo Mbunge wa Kilwa Kusini aliyemaliza muda wake, Suleiman Bungara walikamatwa na Polisi Wilayani Kilwa Juni 23, 2020 kwa kile ambacho Polisi walikiita ‘kuhatarisha amani’.

Kwa mujibu wa Naibu Katibu wa Kamati ya Habari, Uenezi na Mahusiano na Umma, ACT Wazalendo, Janeth Rithe, viongozi hao wametakiwa kuripoti tena Polisi Lindi Julai 20, 2020.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527