
Eng. Sebastian Malunde akichukua fomu ya kuomba ridhaa kugombea ubunge Jimbo la Solwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Vijijini.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mhandisi Sebastian Malunde amechukua na kurudisha fomu ya kuomba ridhaa kugombea ubunge Jimbo la Solwa kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Mhandisi Sebastian Malunde ambaye ni mkazi wa kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga amechukua fomu leo Jumanne Julai 14,2020 majira ya saa mbili na nusu asubuhi na kurudisha fomu majira ya saa nane mchana katika ofisi za CCM wilaya ya Shinyanga Vijijini.
Social Plugin