SHEREHE ZA SIMBA SC KUKABIDHIWA KOMBE LA UBINGWA WA VPL KUFANYIKA JULAI 8,2020


Na Damian Masyenene Shinyanga Press Club Blog
Bodi ya Ligi Tanzania (TPLB) imesema kuwa sherehe za kukabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) kwa klabu ya Simba SC zitafanyika Julai 8, 2020 mjini Ruangwa mkoani Lindi katika Uwanja wa Majaliwa kwenye mchezo wa ligi hiyo dhidi ya wenyeji wake, Namungo FC.

Kwa mujibu wa Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 1, 2020 na Idara ya Habari na Mawasiliano ya Bodi hiyo imesema kuwa sherehe za kukabidhi kombe hilo zitafanyika mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo namba 340.

Soma zaidi taarifa iliyotolewa na TPLB


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527