RAIS MAGUFULI AMPONGEZA DK. LAZARUS CHAKWERA KWA KUCHAGULIWA KUWA RAIS MPYA WA MALAWI


Rais  Magufuli amempongeza Dk. Lazarus Chakwera  kwa kuchaguliwa kuwa Rais mpya wa Malawi. 




Kupitia ukurasa wake wa Twitter; Rais Magufuli amesema, “Nakupongeza Dkt. Lazarus Chakwera kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi.

“Kwa niaba ya Serikali na Watanzania wote, naahidi kuendeleza uhusiano wetu wa kidugu, kirafiki na ujirani mwema hususani katika masuala ya uchumi na ustawi wa jamii. Hongera sana Mhe. Rais,” amesema.

Chakwera amechaguliwa na Wamalawi katika uchaguzi wa marudio uliofanyika tarehe 23 Juni 2020 kwa kupata asilimia 58 akimshinda Rais aliyekuwa madarakani Peter Mutharika.

Uchaguzi huo ulifanyika baada ya ule wa awali wa Mei 2019 kufutwa na mahakama Februari 2020 baada ya kubaini ulikuwa na dosari.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527