MWILI WA RAIS MSTAAFU, BENJAMIN MKAPA KUWASILI MOJA KWA MOJA KIJIJINI LUPASO BADALA YA NACHINGWEA


Mwili wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa utawasili moja kwa moja kijijini Lupaso, mkoani Mtwara kesho jioni kutoka jijini Dar es Salaam tayari kwa maziko yatakayofanyika Julai 29.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa wakati akieleza kuhusu maandalizi ya maziko ambayo amesema hadi sasa yamefikia asilimia 80.

Byakanwa amesema kuwa ratiba imebadilika ambapo awali mwili ulikuwa ushushwe Uwanja wa Ndege wa Nachingwea mkoani Lindi na kisha upelekwa kijijini kwao, lakini sasa utatolewa Dar es Salaam hadi Lupaso.

Amesema taratibu za kuhakikisha kunapatikana malazi na usafiri kwa wageni wote watakaofika bado zinaendelea.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527