ABOUBAKAR JUMA ABOUBAKAR AJITOSA KUGOMBEA URAIS KUPITIA CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI


Ndugu Aboubakar Juma Aboubakar leo Julai 18,2020 ametia nia kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha NCCR-MAGEUZI.


Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa NCCR-Mageuzi, Evarist Komu amemtaka mgombea huyo kupeperusha bendera ya chama kwa kusimamia misingi ya chama hicho ambayo ni pamoja na kutetea utu, haki, udugu, usawa na upendo kwa mustakabali wa chama na Watanzania kwa ujumla.

Abubakar ameahidi kusimamia misingi ya chama chake na kuweka mazingira yatakayokuwa chachu ya kuleta maendeleo endelevu nchini.

Komu amesema hadi sasa wanachama 232 wamechukua fomu za kuomba kugombea ubunge na zaidi ya 3,000 wamechukua fomu za kuomba kugombea udiwani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527