TAKUKURU KUWAHOJI WABUNGE 69 WA CHADEMA KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA ZA CHAMA


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) nchini Tanzania, inatarajia kuwahoji wabunge 69 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuhusu tuhuma za matumizi mabaya ya fedha, 


Taarifa iliyotolewa leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020 na Doreen Kapwani, Afisa Uhusiano wa Takukuru imesema mahojiano hayo yatafanyikia Makao Makuu ya taasisi hiyo Dodoma na yatakamilika wiki ijayo.

“Ni kweli kuwa Takukuru imewaita waheshimiwa wabaunge wa Chadema na waliowahi kuwa wabunge wa chama hicho kwa ajili ya mahojiano.”

“Hatua hii ni muendelezo wa uchunguzi wa malalamiko dhidi ya matumizi mabaya ya fedha nza Chadema unaoendeshwa na Takukuru ambapo hatua iliyopo sasa ni kuwahoji wabunge 69,” amesema Doreen


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527