NYAVU HARAMU 110, KOKORO 2 NA TIMBER 32 ZAKAMATWA NA KUTEKETEZWA BUSEGA


Jumla ya Nyavu 110, kokoro 2 na timber 32 zilizokuwa zinatumika katika uvuvi haram zimekamatwa na kuteketezwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Busega. 


Vifaa hivyo vimekamatwa kati ya tarehe 19/05/2020 na 04/06/2020 katika vijiji vya Nyakaboja kata ya Kabita na Maega Kata ya Kalemela.

Uvuvi haram umekuwa changamoto ukanda wa Ziwa Viktoria, hivyo Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya wilaya ya Busega imeanza kupambana na wavuvi wanaotumia vifaa visivyokubalika kwenye shughuli za uvuvi ili kuzuia uharibifu wa rasimilimali kwenye Ziwa Viktoria.

Kwa upande mwingine Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji imewataka wavuvi wote wilayani humo kufuata sheria za uvuvi kwa kufanya shughuli zao za uvuvi kwa kufuata utaratibu uliowekwa na serikali, kwani uvuvi haram umekuwa moja ya changamoto kwenye ukusanyaji wa mapato yanayotokana na shughuli za uvuvi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527