Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

Rais Magufuli azungumza kwa simu na Rais Mteule wa Burundi Mhe. Evariste Ndayishimiye.

Rais Magufuli amezugumza kwa simu na Rais Mteule wa Burundi Evariste Ndayishimiye na kumpongeza kufuatia uamuzi wa mahakama ya Katiba kuagiza Rais huyo aapishwe haraka.

Katika taarifa iliyotolewa leo Juni 13 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, imeeleza kuwa, Rais Magufuli amemhakikishia Ndayishimiye kuwa Tanzania itaendeleza na kukuza ushirikiano na Burundi.

Aidha Rais Magufuli amerudia kumpa pole Rais huyo mteule kwa msiba wa aliyekuwa Rais wa nchi hiyo Pierre Kurunziza, aliyefariki Juni 9, 2020.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com