Breaking News : RAIS MAGUFULI AMTUMBUA MKUU WA MKOA WA ARUSHA MRISHO GAMBO, DC ARUSHA NA MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Viongozi Watatu Mkoani Arusha na kufanya uteuzi wa viongozi watakaoshika nafasi hizo.
Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na kumteua Idd Kimanta kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha. Pia ametengua uteuzi wa Mkuu wa wilaya ya Arusha mkoani Arusha, Gabriel Daqarro na nafasi yake kushikwa na Kenan Kihongosi. Hali Kadhalika ametengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Dkt. Maulid Madeni na kumteua Dkt. John Pima kushika nafasi hiyo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527