IRAN YATOA WARANTI YA KUKAMATWA RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP


Iran imetoa waranti wa kukamatwa Rais wa Marekani Donald Trump na wanajeshi 35 wa Marekani, ikiwa ni pamoja na maafisa kutoka taifa hilo kwa kuhusika na kifo cha Jenerali Qassem Soleimani.

Iran pia imeomba msaada wa polisi ya kimataifa ya Interpol kuhusu faili hiyo, ofisi ya mashitaka ya Tehran imetangaza leo Jumatatu, kulinganan nashirika la habari la FARS.

Jenerali Qassem Soleimani alikuwa mkuu wa kikosi cha Quds, kitengo cha Walinzi wa Mapinduzi wa Irani, aliuawa mwezi Januari mwaka huu katika shambulio la anga la Marekani nchini Iraq kwa ombi la haraka la rais Donald Trump.

Waranti huo umemuhusisha Trump kwa "mauaji" na "hatua ya ugaidi," amebaini mwendesha mashtaka wa Tehran Ali Alqasimehr, akinukuliwa na shirika la habari la FARS.

Ameongeza kuwa Iran imeomba polisi ya kimataifa, Interpol, kutoa "notisi nyekundu" dhidi ya Donald Trump na wengine ambao Tehran inaona kuwa walihusika katika kifo cha Qassem Soleimani.

Washington inamshutumu Qassem Soleimani kwa kupanga njama za kufanya mashambulizi dhidi ya kambi za muungano wa kijeshi unaoongowza na Marekani nchini Iraq.

Akiwa mkuu wa kikosi cha Quds Soleimani alisimamia operesheni za kijeshi nje ya Iran na kuingia kweny euhasama na Marekani wakati wa vita vya Iraq akionekana kuwa mfadhili wa makundi ya wanamgambo wa kishia.

Marekani ilikilaumu kikosi cha Quds kwa shambulizi la Karbala lililowauwa wanajeshi wake watano pamoja na kutoa mafunzo na watengenezaji mabomu yaliyiotumika kuvilenga vikosi vyake.

Mwaka 2007 Marekani na Umoja wa Mataifa walimjumuisha Soleimani katika orodha ya watu waliowekewa vikwazo lakini aliendelea kusafiri maeneo mbali mbali duniani.

Umaarufu wake uliimarika zaidi wakati wa vita vya Syria na kutanuka kwa kundi linalojiita dola la kiislam. Iran ilimtuma Soleimani mara kadhaa nchini Syria kuongoza mashambulzi dhidi ya kundi la IS na makundi yanayopinga utawala wa Bashr Al Assad.

Jenerali huyo alipata mafanikio makubwa kwenye mapambano ya ardhini na alikuwa alama ya ushindi katika vita dhidi ya IS na kuendelea kulipa nuru jina lake.

-RFI


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527