SERIKALI YA TANZANIA YATOA TAARIFA MWENENDO WA CORONA


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema kuwa, idadi ya wagonjwa wa Corona hapa nchini imepungua kwa kiasi kikubwa na kubaki na wagonjwa wanne pekee walio katika Mkoa wa Dar es Salaam.

Waziri Ummy ameyabainisha hayo leo Juni Mosi, 2020, wakati wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, ya uzinduzi wa jengo la Bodi ya Mkonge lililopewa jina la Mkonge House, na kusisitiza kuwa kwa takwimu hizi watu wasijisahau, bali waendelee kujikinga na ugonjwa huo.

"Hapa Tanga hatuna mgonjwa wa Corona, DSM katika Hospitali ya Amana wamebaki 3, Mloganzila 1, Kibaha hatuna mgonjwa, Mwanza hatuna mgonjwa jambo la kusisitiza ni kuwa Corona bado ipo tuendelee kujikinga, na mimi nilisema pale Ikulu Dodoma katika Uwaziri wangu sikuwahi kupitia kipindi kigumu kama hiki cha Corona kwakweli nilihenya" amesema Waziri Ummy.
Via >> EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527