WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAFIKA 700


Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona nchini Kenya imeongezeka hadi 700 baada ya wagonjwa wapya 28 kuthibitishwa katika kipindi cha saa 24.


Katibu mtendaji katika wizara ya Afya Rashid Aman amesema kwamba kati ya wagonjwa hao wapya 10 wanatoka Momabasa , 9 kutoka kajiado na 7 kutoka Nairobi huku 2 wakitoka Wajir.

Wagonjwa wote tisa kutoka Kajiado ni Wakenya ambao ni madereva wa malori ya masafa marefu ambao walipimwa katika mpaka wa Namanga.

Jumla ya sampuli 841 zilifanyiwa vipimo katika kipindi cha saa 24 zilizopita

Afisa huyo wa afya ametangaza wagonjwa wengine 12 waliopona na hivyobasi kufanya idadi ya wale waliopona kufikia 251.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527