RC MAKONDA ATOA OFA YA NGUO KWA WAKAZI DAR ILI WASHEREKEE VIZURI DISKO LA KUIKABILI CORONA


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ametangaza Punguzo kubwa la Bei ya Nguo la hadi 80% kwenye Maduka Makubwa ya Nguo yaliyopo Jijini humo ili kuhakikisha Wananchi wanapendeza na kuwa nadhifu Jumapili ya May 24 kwenye Kilele cha Siku Tatu za Shukrani Kwa Mungu zilizotangazwa na Rais Dkt. John Magufuli.

RC Makonda amesema atafurahi kuona kila mwananchi wa mkoa huo anasheherekea kwa nderemo na vifijo siku ya jumapili kama sehemu ya shukrani kwa Mungu kwa kutukinga na Corona na baada ya hapo kila mmoja achape kazi ili kwa pamoja tuinue Uchumi wa Taifa.

Pamoja na hayo RC Makonda ametangaza Shindano la DJ bora ambapo kila DJ atatakiwa kumtumia Video Clip huku akiwaelekeza wenye Bar, Hotel, Lodge, Band na Biashara kuzifungua.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527