MAKAMU RAIS WA KWANZA WA SUDANI KUSINI RIEK MACHAR NA MKE WAKE WAAMBUKIZWA CORONA


Makamu Rais wa kwanza wa Sudani Kusini Riek Machar na mke wake Angelina Teny wamethibitishwa kuambukizwa virusi vya corona.

Dkt. Machar alisema kwamba yeye na mke wake ambaye pia ni waziri wa ulinzi, wamepata maambukizi baada ya kutangamana na jopo la ngazi ya juu la kukabiliana na virusi hivyo nchini humo.

Machar amesema kwamba hana dalili zozote na hali yake ya afya iko sawa lakini atajiweka karantini kwa siku 14.

Wengine waliothibitishwa kuambukizwa ni walinzi kadhaa na wafanyakazi.

Mpaka sasa Sudan Kusini imerekodi waathirika 236 na vifo vinne


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527