Picha : MSAMBAZAJI WA GESI 'KIBIRA GAS' ATOA MSAADA WA VIFAA VYA KISASA KUKABILIANA NA CORONA KWA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA SHINYANGA

Msambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC),Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.


Na Estomine Henry - Mratibu SPC
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ ametoa msaada wa vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC).

Msambazaji huyo wa Gesi Maarufu ‘Kibira Gas’ amekabidhi vifaa hivyo kwa Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga, Kadama Malunde leo Jumamosi Mei 2,2020 katika ofisi ya SPC iliyopo Mjini Shinyanga.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo zikiwemo sabuni 5 za maji,tishu 6,ndoo mbili,barakoa,beseni moja na kifaa cha kisasa cha kunawia mikono kwa kukanyaga, Kibira amesema vifaa hivyo vitawasaidia waandishi wa habari kukabiliana na maambukizi ya Virusi vya Corona wanapotekeleza majukumu yao ya kuhabarisha jamii.

“Nimewiwa kufika hapa kuwachangia vifaa hivi kwani Waandishi wa habari ni miongoni mwa makundi ambayo yapo hatarini kupata maambukizi ya Virusi vya Corona kutokana na shughuli zao ambazo zinafanya wakutane na watu mbalimbali kila siku”,amesema Kibira.

Naye Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde amemshukuru Kibira kwa msaada huo akibainisha kuwa amekuwa mdau wa kwanza mkoani Shinyanga kuliangazia kundi la waandishi wa habari ambao kutokana na kazi yao wanahitaji vifaa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona.

“Tunamshukuru sana mdau wetu Kibira Gas kwa msaada huu ambao tunaamini utaongeza nguvu katika mapambano dhidi ya virusi vya Corona”,amesema Malunde.

Katika hatua nyingine Malunde amewakumbusha waandishi wa habari kuzingatia maelekezo yanayotolewa na serikali kuhusu ugonjwa wa Corona na kuhakikisha wanachukua tahadhari kwa kuepuka mikusanyiko,kuvaa barakoa,kunawa maji tiririka na sabuni pamoja na matumizi ya Sanitizer.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC),Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Mei 2,2020 -Picha zote na Marco Maduhu na Frank Mshana.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akionesha namna ya kunawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa wakati akimkabidhi Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde (kulia)vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga ,Kadama Malunde akinawa mikono kwa kutumia kifaa cha kisasa kilichotolewa na Kibira Gas kwa ajili ya waandishi wa habari mkoani Shinyanga kujikinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona.
Kushoto ni Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (SPC) ,Kadama Malunde akimshukuru Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ kwa msaada wa vifaa vya kisasa vya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Corona kwa waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga leo Jumamosi Mei 2,2020. Kibira pia ametoa msaada wa Barakoa maalumu zenye nembo ya Malunde 1 blog kwa waandishi wa habari wa mtandao wa Malunde 1 blog
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ (kushoto) akipiga picha ya kumbukumbu na Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde ambaye pia ni Mkurugenzi wa Malunde 1 blog baada ya kumkabidhi barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog kwa ajili ya waandishi wa habari wa Mtandao wa Malunde 1 blog
Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’ (katikati) akipiga picha ya kumbukumbu na Mwenyekiti wa SPC, Kadama Malunde ambaye pia ni Mkurugenzi wa Malunde 1 blog na Mwandishi wa Malunde 1 blog , Marco Maduhu (kushoto) baada ya kumkabidhi barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog kwa ajili ya waandishi wa habari wa Mtandao wa Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Malunde 1 blog  Kadama Malunde (kulia) na Mwandishi wa Malunde 1 blog , Marco Maduhu (kushoto) wakiwa wamevaa barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Barakoa maalumu zenye Nembo ya Malunde 1 blog zilizotolewa na Mfanyabiashara maarufu anayejihusisha na Usambazaji wa Gesi katika Manispaa ya Shinyanga Sadiki Idrisa Kibira ‘Kibira Gas’.
Picha zote na Marco Maduhu na Frank Mshana.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post