Picha : POLISI SHINYANGA WAKAMATA WATU 48 MATUKIO YA WIZI,UGANGA BILA KIBALI...ANGALIA MALI ZILIZOIBIWA



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga - Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha pikipiki zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zingine zikidaiwa kutumika katika matukio ya uhalifu zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mali mbalimbali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi zilizokamatwa  wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020 katika wilaya ya Shinyanga 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba akionesha mapipa matatu na mtambo wa kutengeneza pombe ya Moshi.

Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog


Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limefanikiwa kukamata watuhumiwa 48 wa makosa mbalimbali wakiwa na mali zinazodhaniwa kuwa ni za wizi katika wilaya ya Shinyanga.

Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari Aprili 9,2020,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema watuhumiwa hao wamekamatwa wakati wa Misako na Operesheni mbalimbali zilizofanywa na Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga katika kipindi cha kuanzia Mwezi Desemba 2019 hadi Machi,2020.


Kamanda Magiligimba amesema kati ya watuhumiwa hao 48 wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya kuvunja nyumba na kuiba,kupatikana na mali zidhaniwazo kuwa ni za wizi,kufanya shughuli za uganga bila kibali, kukamatwa na bangi,mirungi,pombe ya moshi na tuhuma mbalimbali, 

Amesema watuhumiwa 28 wamefikishwa mahakamani na 20 bado wapo chini ya upelelezi.

Amezitaja mali zilizokamatwa kuwa ni Magodoro 7,TV 9, pikipiki 4,baiskeli 5,sabufa 3, vitenge pea 9,Laptop 4,pasi moja ya umeme,Inverter moja,CPU 2 na King’amuzi kimoja.

Vingine ni Bangi mafurushi matatu,mirungi mabunda 32,sabuni B29 Boksi 3, mchele kilo 43.5 na vifaa vya kufanyia shughuli za uganga na mapipa matatu na mtambo wa kutengeneza pombe ya Moshi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527