RAIS PUTIN WA URUSI AAAMURU WATU WA NCHI HIYO KUTOKWENDA KAZINI NA KUBAKI MAJUMBANI KUKABILIANA NA CORONA


Rais wa Urusi Vladimir Putin ameamuru raia wa nchi hiyo kutokwenda kazini na kusalia nyumbani hadi mwishoni mwa mwezi Aprili kama sehemu ya juhudi za kuzuia kusambaa kwa virusi hatari vya corona.

Akilihutubia taifa kwa njia ya televisheni, Putin amesema anarefusha sera ya kutofanya kazi kwa muda wa wiki tatu zaidi na wafanyakazi wote wanapaswa kulipwa mishahara ndani ya kipindi hicho.

Putin amesema baadhi ya viwanda vinavyozalisha bidhaa muhimu vitaendelea kufanya kazi na maduka ya vyakula na dawa yanaruhusiwa kufunguliwa.

Kiongozi huyo ameongeza kuwa mkakati wa Urusi wa kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona umefanikiwa lakini ameonya kuwa idadi ya watu walio na maambukizi ya virusi hivyo itaendelea kuongezeka.

Hadi kufikia Alhamisi Urusi imerikodi visa 3,548 vya wagonjwa wa COVID-19 pamoja na vifo vya watu 30


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527