MARUFUKU YA KUTOTOKA NJE USIKU NCHINI KENYA YAONGEZWA KWA SIKU 21..WAGONJWA WA CORONA NCHINI WAMEFIKA 343


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ameongeza muda wa marufuku ya watu kusafiri na kuingia au kutoka katika mji wa Nairobi na miji mingine minne kwa muda wa siku 21 ili kuendelea kukabiliana na Virusi vya Corona.

Marufuku ya kutoka nje nyakati za usiku kwa taifa zima pia imeongezwa kwa siku 21.
 
Kenyatta  ametangaza kuwa Kenya sasa ina visa 343 baada ya wengine 7 kuongezeka leo  na wagonjwa waliopona ni 94


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527