MAMLAKA YA HALI YA HEWA NCHINI (TMA) YATOA TAHADHARI YA MVUA KUBWA


Mamlaka ya Hali ya Hewa Nchini (TMA), imetoa tahadhari ya kunyesha kwa Mvua kubwa ndani ya siku nne kuanzia leo Aprili 17, 2020.

Tahadhari hiyo imetolewa jana Alhamisi Aprili 16, 2020 jijini Dar es Salaam na Meneja wa Kituo  Kikuu cha Utabiri wa Mamlaka hiyo, Samwel Mbuya  ambae amesema amesema mvua hiyo ya siku nne inatarajia kunyesha kuanzia ya April 17 hadi 20 mwaka huu.

Aidha ametaja maeneo yanayotarajia kupata vipindi vya mvua kubwa ni pamoja na Mkoa wa Pwani ,Kisiwa cha Mafia ,Tanga, Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post