WAUGUZI WA WAGONJWA WALIOMBUKIZWA VIRUSI VYA CORONA KENYA WAANZA MGOMO BARIDI

Wauguzi wanaofanya kazi katika wodi iliyotengwa kwa watu walioambukizwa virusi vya corona nchini Kenya wameanza mgomo baridi kulalamikia kile wanachodai kuwa ukosefu wa vifaa vya kujikinga na mafunzo ya kutosha.


Hospitali ya Mbagathi katika mji mkuu wa Nairobi, ni moja ya hospitali zilizo na wodi ya kutibu wagonjwa waliombukizwa virusi hivyo hatari.

Katibu mkuu wa muunganowa wauguzi nchini Kenya,Seth Panyako ameiambia BBC kwamba wauguzi watarejea kazini ikiwa watapewa mavazi maalum na mafunzo ya jinsi ya kuwashughulikia wagonjwa.

Credit -BBC


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527