WANAOONGEZA BEI VIFAA VYA KUJIKINGA NA CORONA KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA


Serikali imeiagiza Tume ya Ushindani wa Kibiashara na Shirika la Ubora wa Viwango (TBS) kufanya msako na kuwachukulia hatua wafanyabiashara watakaobainika kuongeza bei kwa makusudi kwa lengo la kujipatia faida kubwa katika kipindi hiki kigumu cha mapambano dhidi ya virusi vya Corona.

Agizo hilo limetolewa leo Machi 21, 2020 na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa ambapo pia amewaonya wafanyabiashara walioficha bidhaa za vitakasa (sanitizers) na barakoa (mask) kuacha mara moja huku akiwatoa hofu Watanzania kuhusu upatikanaji wa bidhaa hizo na kuongeza kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha bidhaa zinapatikana kirahisi na kwa bei nafuu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post