RAIS MAGUFULI AMTEUA BRIGEDIA JENERALI MBUNGO KUWA MKURUGENZI WA TAKUKURU



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Brig. Jenerali John Mbungo kuwa Mkurugenzi wa taasisi hiyo kwa kazi nzuri aliyoifanya ikiwemo ya kurejesha bilioni 8.8 walizodhulumiwa wananchi.

Rais amefanya uteuzi huo leo, Machi 26, 2020 katika hafla ya kupokea ripoti kutoka Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali CAG na ripoti ya TAKUKURU katika Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post