STAA WA MUZIKI WA SOUKOUS KUTOKA DR CONGO, AURLUS MABÉLÉ AFARIKI DUNIA


Staa na nguli wa muziki wa Soukous kutoka DR Congo, Aurlus Mabélé amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 67. 


Chanzo cha kifo chake bado hakijawekwa wazi lakini Mabélé alikuwa akisumbuliwa na Saratani (cancer) kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa mwanamuziki Nyboma Mwandido, Mabele amefariki usiku wa kuamkia leo katika Hospitali moja jijini Paris Ufaransa.

Nyboma amesema Mabele alilazwa hospitalini Alhamis Machi 19, 2020 usiku.

Sababu rasmi ya kifo chake bado haijawekwa wazi huku vyanzo mbalimbali vikieleza huenda ni Corona na vingine vikisema ni mshtuko.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527