RWANDA YATANGAZA MIKAKATI KABAMBE YA KUKABILIANA NA VIRUSI VYA CORONA....MIPAKA YOTE IMEFUNGWA, BAA, KUSAFIRI HOVYO MARUFUKU

Wakati ugonjwa wa virusi vya corona  ukiwa unaenea kwa kasi katika maeneo mbalimbali ulimwenguni,Waziri mkuu wa Rwanda Dkt.Ngirente ametoa maagizo 10 ya kukabiliana nao.

Baadhi ya maagizo aliyoyatoa Dkt.Ngirente ni pamoja na kutoruhusu safari zisizo za lazima,malipo ya kieletroniki zaidi yatatumika kuliko kutumia ATM ,Waajiriwa/Watumishi wote wa umma na sekta binafsi watafanya kazi wakiwa majumbani isipokuwa wale watoa huduma muhimu.

Maagizo mengine ni mipaka yote kufungwa,isipokuwa usafiri wa mizigo,safari kati ya miji na wilaya tofauti ndani ya nchi hairuhusiwi isipokuwa kwa sababu za matibabu,usafirishaji wa chakula au bidhaa muhimu zitaruhusiwa.

Pia Dkt.Ngirente ameagiza maduka na masoko yote kufungwa  isipokuwa yale yanayouza chakula,Dawa, vifaa vya usafi huku baa zote zikifungwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527