JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO YARIPOTI KIFO CHA KWANZA KUTOKANA NA CORONA NA VISA VITANO VIPYA


Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo leo imeripoti kifo cha kwanza kutokana na virusi vya corona pamoja na visa vitano vipya vya maambukizi.Kupitia mtandao wa twitter, waziri wa afya nchini humo Eteni Longondo, amethibitisha kifo hicho kilichotokea hapo jana pamoja na visa hivyo vipya akisema wote walioathirika ni raia wa Congo na kwamba maafisa wake wanawashughulikia. 

Nchi hiyo imeripoti visa 23 kwa jumla tangu Machi 10 na kifo hicho kinaongeza idadi ya waliofariki kutokana na virusi hivyo katika eneo la jangwa la Sahara barani Afrika kufikia watu watatu baada ya vifo vilivyoripotiwa wiki hii katika nchi za Burkina Faso na Gabon.

Hapo jana, serikali ya Congo, iliratibu mikakati ya kinga hasa katika mji mkuu Kinshasa ambao ni makazi ya takriban watu milioni 10 na ambapo ndiko kwenye visa vingi vya virusi hivyo kwa sasa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527